Sunday, June 5, 2011

Serengeti High Way Part 4




________________________________________
Sehemu ya Nne
Wapendwa wasomaji, kama nilivyowahadi toleo la leo limelenga kukupa habari za hivi karibuni toka wilaya zinazopakana na Hifadhi ya Serengeti.Mapema Mei mwaka huu Bodi ya barabara ya Mikoa ya Arusha na Mara walikutana na wadau wa Mamlaka ya Hifadhi Tanzania(TANAPA) na kukubaliana kuwa ni lazima barabara hiyo ijengwe kama vile serikali ilivyopanga lakini kwa kuzingatia ulinzi wa mazingira.Wakizungumza wakati wa mkutano wa Bodi hiyo ya barabara Meneja wa TANROAD , Bwana Desdatus Kaboko alisisitiza kuwa kuanzia January tayari wameshaanza kukusanya pesa za mradi huu na wanategemea uanze rasmi mwaka 2012.Mkutano huo ulionyesha kuwa barabara ile ni muhimu sana kwa mapinduzi ya kiuchumi kwa wakazi wa mikoa hiyo na kanda ya ziwa.Pia TANAPA ambayo awali ilikuwa inapinga mpango wakati huu inaonekana kuwa pamoja na serikali katika juhudi za kuwakwamua wananchi kimaendeleo bila kuharibu mali asili yoyote.
Tarehe 31 mwezi Mei 2011 Mkurugenzi wa Benki ya Dunia Tanzania na Uganda Bwana John Murray pamoja na Mwakilishi wa Balozi wa Ujerumani ,Gisela Habel walitembelea wilaya ya Ngorongoro na Kufanya mikutano na wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro.Mwakilishi huyu aliongozana pia wataalamu wa barabara na mazingira wa bank hiyo, viongozi toka wizara ya Ujenzi na viongozi wa TANROAD Mkoa wa Arusha.
Bahati nzuri nami nilikuwepo Wilayani Ngorongoro kwa shughuli mbalimbali na kuweza pata taarifa hizi kwa undani.Wananchi wa Wilaya hii japo sio wote walifanikiwa kufanya mkutano na viongozi hao na kueleza dukuduku zao.Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kupata mawazo ya wananchi juu ya barabara ya Musoma -Loliondo hadi Arusha.Mkutano huo ulifanyanyika katika Kijiji cha Soit sambu-loliondo.Msafara huo ulipokelewa na mabango yanayosisita kuwa barabara ya lami ni muhimu kwa maendeleo ya wanangorongoro.Baadhi ya Mabango ya hayo yakuwa na ujumbe ufuatayo;

"Huduma hi ya barabara itasadia huduma mbalimbali za maendeleo kama vile zahanati, shule na Afya"

Pia bango lingine lilijidadi kuwa; " Tunahitaji barabara ya lami wa maendeleo ya wanangorongoro"
Wananchi wengi walimweleza Mkurugenzi huyo kuwa barabara ya lami ni muhimu kwa maendeleo hasa hupatikanaji wa masoko ya mifugo na biashara zingine.Wanachi hao walionyeshwa kukerwa na watu wanaopinga barabara ambao ni mpango wa serikali kuwakwamua wananchi wake kiuchumi.Waliwalaani wale wote hasa wanaotoka mataifa ya nchi na kupinga mpango huu wa barabara.




Wanagorongoro wakimpokea Mkurugenzi wa World Bank kwa Mabango

Nao viongozi mbalimbali wa wilaya hasa madiwani walieleza kuwa hatuko tayari kuona maslahi ya wananchi yakibinywa na wachache wenye maslahi binafsi.Diwani wa Soit Sambu Daniel Ngoitiko alionekana kukerwa na wanaharakati pamoja na mashirika ya nje yanayopinga barabara ilihali katika nchi zao barabara za lami zimepita katika mbuga zao.Mhe Daniel Ngoitiko aliendelea kuitaka serikali isiyumbishwe na kelele za mashirika pamoja na nchi mbalimbali zinazotaka kupindisha barabara hii ipite mahali kwingine.Kwa ujumla wananchi na viongozi wao wilayani Ngorongoro wamesema barabara ni haki yao na hakuna mtu yoyote anaeweza pinga mpango huo ambao uberakiwa na Bunge la Tanzania na madiwani wa Mikoa yote inayozunguka hifadhi ya Serengeti.

Walindelea kusema kwa sasa hatutakubali kuona wananchi wa wilaya hizi tunaendelea kuachwa nyuma kimaendeleo wakati wengine wanazidi kusonga mbele kimaendeleo.Walinukuu katikaba na kusema katiba ya Tanzania inasema Taifa linajukumu ya kutoa fursa sawa za maendeleo kwa watu wake
bila ubaguzi au upendeleo na rasilimali za nchi zitumike sawa kuleta maendeleo kwa wote.Wananchi hawa waliendelea kusema "tumenyasasika na kusahaulika kwa muda mrefu lakini leo baadhi ya watu wachache wanataka hata barabara tusipate" alisema mmoja wa wanavijiji

Ukweli ni kwamba wanachi wale wanahitaji vichocheo vya maendeleo kama vile barabara na umeme ili kuwatoa kwenye lindi la umaskini.Wanachi wale wametunza maliasili yote, lakini leo hawathamniki tena wanaitwa wakenya na wavamizi.Sasa inakuwaje leo msimame na kupinga barabara ambayo inaweza kuwa chanzo cha mabadiliko.Hakika mnaopinga barabara ya Musoma-Arusha hamna nia njema na wananchi wa wilaya hizi zilizoachwa nyuma kimaendeleo.

Naye mwakilishi wa WB Tanzania aliwaeleza wananchi wale kuwa hana tatizo na barabara hii na Benki ya Dunua ipo tayari kusaidia kama ni vipaumbele vya wanachi na Taifa lake.Pia viongzi wengine wa kitaifa akiwemo Meneaja wa TANROAD Arusha aliwaakishia kuwa mpango wa barabara bado upo pale na hakuna atayeweza kuutengua.
Ni wazi kuwa jamii hizi kwa miaka mingi zimetengwa na ulimwengu mwingine kimaendeleo.Watu wametumia vigezo vya vyanzo vya utalii kuwanyima wananchi hao maendeleo mbalimbali.Wananchi hawa wametunza mali asili zote hizi bila kuona faida kubwa ya utunzaji huu.Hakuna shirika lililowahi kuja na kujaribu kufanya tathmini ili kuona ni kwa kiasi gani wananchi wale wamenufaika na rasilimali hizo.
Wananchi hawa wamekuwa nyuma kielimu na kimaendeleo na sasa ni wakati muafaka kuruhusu barabara hii iwe kichecheo cha mabadiliko ya maisha ya wananchi wanaozunguka hifadhi hii ya Seregeti.Ni wazi kwamba barabara hii ikisimamiwa vizuri itafungua mianya mingi ya maeondeleo kwa wanachi wa mikoa yote miwili.
Mfano Wananchi wanaoshi Tarafa ya Ngorongoro Wilayani Ngorongoro kwa muda mwingi wamenyimwa kujishugulisha na shughuli zingine za kimaendeleo mbaya zidi hata fedha wanazopata kama mgawo wa mapato ya mamlaka ya Ngorongoro ni ndogo na nyingine huishia kuliwa na wajanja. Kama mtu halimi, hajaenda shule, hafanyi biashara na hana mahala pa kuchungia mifugo , je maisha yake ya baadaye yatakuwaje?
Kwa muda mwingi sasa wananchi wa wilaya za Ngororngoro na Serengeti wamekuwa wakirubiniwa na vipesa vidogovidogo hasa kupitia baadhi ya viongozi wao kuruhusu maeneoa yao yapokonywe.Mfano Loliondo kwa sasa Kampuni ya Thomson Safari inaendelea kujitanua katika ardhi ya vijiji kwa kutumia baadhi ya madiwani waroho wa madaraka na pesa.Wananchi kwa sasa wamechoka na vitendo vya ardhi yao kuporwa na kupewa wawekezaji na kuwafanya wao wakimbizi ndani ya ardhi yao.Mtakumbuka kuwa wananchi wengi walipinga kuwepo kwa makpuni ya OBC na Thomson katika ardhi yao ya malisho.Jitihada hizi zilishia wengi kupigwa risasi na wengine kuishia mikononi mwa polisi.
Mazingira kama haya ndio yanawafanya wanachi sasa wafikirie njia mbadala ya kujikwamua kimaendeleo baada ya kuona hawana tena maeneo makubwa ya ufugaji.Tukumbuke kuwa kwa sasa hali ya ukame ni tishio na pia maeneo makubwa yameshikiliwa na makampuni na hoteli za kitalii wilayani Serengeti na Ngorongoro.
Kuwepo kwa barabara hii itasaidia wanachi wale kubadilika na kujaribu kufanya shughuli zingie za kimaendeleo kama vile biashara.Pia Barabara hii itasaidia kwa kiasi kubwa kufungua soko la mifugo na mazao ya mifugo kama vile ngozi na nyama.


Ndugu msonaji hiyo ndio hali halisi na maoni ya wananchi, Benki ya Dunia pamoja na
TANROAD juu ya barabara ya Musom-Loliondo-Arusha.Soma Toleo la Tano.

By Onesmo Olengurumwa
Vice President Ngorongoro Elites Association NDUSA-ndusa@gmail.com

1 comment:

Masegeri said...

Kaka asante sana kwa hii taarifa nzuri.Itakuwa vyema sana kama ukiaindaika kwa kiingereza halafu tukai-post kwenye webpage ya STOP THE SERENGET HIGHWAY ambapo ndio kuna watu wengi wanaoipinga hii barabara.Wengine hata wanathubutu kusema eti wananchi wa ngorongoro hawaitaki hii barabara,ni serikali ndo inawalazimisha.Pia kwenye hiyo webpage yao utaona comments zangu nyiongi ambazo nimekuwa nikipingana na hao watu hadi tumegombana sana.Fuatilia hili suala kwa hii link:http://www.facebook.com/#!/topic.php?uid=125601617471610&topic=146